Skip to main content

#03.Bible in relation to Singing(Sacred Songs).


Awali niliweka mtiririko kadhaa kuonesha Namna Biblia inavyoelezea suala la #Uimbaji na #Utunzi wa Nyimbo Tak.
Leo nitaweka nyongeza ya mstari wa Biblia unaoelezea uwezo wa nyimbo/muziki mtakatifu kuleta uwepo na ufunuo wa Mungu mahali unapoimbwa,huu utakuwa Ni muendelezo wa tatu unaohusiana na ule wa kwanza na wa pili:
Rejea kitabu Cha "Mambo ya Nyakati.5:12-14.{2 Chronicles.5:12-14}.
Biblia imeandika;
"tena Walawi waimbaji, wote pia, yaani, Asafu, na Hemani, na Yeduthuni, na wana wao, na ndugu zao, hali wamevaa kitani safi, wenye matoazi na vinanda na vinubi, wamesimama upande wa mashariki wa madhabahu, na pamoja nao makuhani Mia na ishirini wakipiga panda ;hata ikawa, wenye panda na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakasikizisha sauti moja ya kumsifu Mungu na Kumshukuru Bwana, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele; NDIPO NYUMBA YA BWANA IKAJAWA NA WINGU, NAAM, NYUMBA YA BWANA, hata makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya lile wingu; KWA KUWA NYUMBA YA MUNGU IMEJAA UTUKUFU WA BWANA."
Biblia ipo wazi kabisa, Mara Tu Baada ya waimbaji (na wapigaji-mstari wa 13) kuanza kazi yao NDIPO...nyumba ya Bwana ikajawa na Wingu(lililoashiria Utukufu wa Bwana-mstari wa 14).
Msisitizo Ni uleule...UPO UHUSIANO KATI YA;
•UIMBAJI(Kwaya na Nyimbo nyingine za Ibada), AU
• UTUNZI-(ukirejea mtiririko wa kwanza na wa pili),
  PAMOJA NA UWEPO/UTUKUFU WA MUNGU PINDI nyimbo iliyotungwa ikiimbwa mahali husika.
*Suala Si KUTUNGA NYIMBO TU ama KUIMBA MYIMBO TU...SUALA NI:
"JE????UTUKUFU WA MUNGU UNAONEKANA PINDI NYIMBO HUSIKA INAPOWASILISHWA MAHALI?"
"Je???Nyimbo tunazotunga na kuimba zina NGUVU KIASI GANI KULETA MABADILIKO KWA MUIMBAJI NA MSIKILIZAJI?

*Mtiririko unaokuja nitaweka tafsiri ya mistari hapo juu kwa lugha ya Kiingereza(ili kuongeza upana wa maarifa) Kisha tutapata Uelewa na kinachomaanishwa.
nikutakie tafakari njema.

Anophrine D.S.
@Mzumbe University.

Comments

Popular posts from this blog

Biblia inasema nini kuhusu utunzi wa nyimbo takatifu?[#02]

Ndugu katika Kristo,Mwokozi wetu apewe sifa.... Leo tunaendelea na mtiririko wa pili(2) wa somo letu.Katika Mtiririko uliopita tulitoa utangulizi wa Neno kutoka kitabu cha "Kumbukumbu la Torati.31:19-22,30." Leo nitatolea ufafanuzi kuhusu mistrari hii; Jambo la umuhimu la kuona hapa ni kupitia mstari wa 19...Mungu anamwambia Musa "ANDIKA WIMBO HUU" ,katika Biblia ya kiingereza chepesi(Bible in Basic English) ,Neno lililotumika badala ya neno 'andika' ni neno 'tengeneza/kamilisha' ,Kutokana na hayo tuelewe yafuatayo; >Ni jambo la muhimu kwa watunzi/waimbaji kutotengeneza wimbo/nyimbo kwa utaratibu tunaoutaka sisi Bali kwenda kwa gwiji wa Muziki Mtakatifu{ndiye Mungu mwenyewe},ili atupe wimbo/nyimbo yeye mwenyewe[kwa kuwa Musa aliambiwa "ANDIKA" ,Hakujiamulia peke yake]. Fahamu ya kuwa Nyimbo inayotoka kwa Mungu kwenda kwa mtunzi inabeba nguvu(upako) unaoelezewa katika mstari wa 21 kuwa; (a)unakuwa SHAHIDI(ukishuhudia ndani y...

Biblia Takatifu inasema nini kuhusu utunzi wa nyimbo Takatifu{Sacred songs}??!

Wapendwa katika Krisro Yesu ,Tumsifu Mwokozi wetu............... ~Kwa kitambo kirefu nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa ,likiwemo Hili ambalo nimeliweka kama kichwa cha muhtasari huu;'Biblia Takatifu inasema nini/inatufundisha vipi kuhusu utunzi[uandishi] wa nyimbo Takatifu?'. Hatimaye nimefanikiwa kupata mwangaza kidogo kulihusu jambo Hilo ,na majibu yake Ni ndani ya kitabu hikihiki tunachotembea nacho kila siku(Biblia Tak.). Nitatoa chambuzi hizi katika mfululizo wa masomo(vipindi)kadhaa na kwa kuanza na mtiririko wa kwanza nitakuonesha[ewe mtunzi wa nyimbo Tak.] mistari katika Biblia ,Kisha katika mtiririko wa pili nitaitolea ufafanuzi; Rejea 'Deutoronomy.31:19,21,22&30[Kumbukumbu la Torati.31:19,21,22&30] ,Biblia inasema;(nitatoa nukuu ya kiingereza na kiswahili pamoja): "And now write this song for yourselves and teach it to the Israelites;put it in their mouths, that this song may be a witness for me against the Israelites. And when many evil...

Tumsifu Yesu Kristo.........

Ni tumai langu kuwa nyote mu wazima ,Napenda kukukaribisha katika ukurasa huu, Ni wazo nililokuwa nalo toka kitambo ,kuanzisha ukurasa ambamo kupitia humo nitaweza kuweka mambo muhimu yanihusuyo kama vile nota za tunzi alizoniwezesha Mungu kuzitengeneza ,mashairi n.k ambayo yote kwa ujumla yanaweza kuwa ya msaada kwetu sote ili kulijenga kanisa la Mungu. Huu Ni mwanzo tu ,na taratibu ukurasa huu utakamilika hatua kwa hatua kadiri atakavyowezesha Roho Mtakatifu aliyeianzisha kazi hii. Asante! Anophrine Desdeus Shirima.