Skip to main content

Biblia Takatifu inasema nini kuhusu utunzi wa nyimbo Takatifu{Sacred songs}??!

Wapendwa katika Krisro Yesu ,Tumsifu Mwokozi wetu...............
~Kwa kitambo kirefu nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa ,likiwemo Hili ambalo nimeliweka kama kichwa cha muhtasari huu;'Biblia Takatifu inasema nini/inatufundisha vipi kuhusu utunzi[uandishi] wa nyimbo Takatifu?'.
Hatimaye nimefanikiwa kupata mwangaza kidogo kulihusu jambo Hilo ,na majibu yake Ni ndani ya kitabu hikihiki tunachotembea nacho kila siku(Biblia Tak.).
Nitatoa chambuzi hizi katika mfululizo wa masomo(vipindi)kadhaa na kwa kuanza na mtiririko wa kwanza nitakuonesha[ewe mtunzi wa nyimbo Tak.] mistari katika Biblia ,Kisha katika mtiririko wa pili nitaitolea ufafanuzi;
Rejea 'Deutoronomy.31:19,21,22&30[Kumbukumbu la Torati.31:19,21,22&30] ,Biblia inasema;(nitatoa nukuu ya kiingereza na kiswahili pamoja):
"And now write this song for yourselves and teach it to the Israelites;put it in their mouths, that this song may be a witness for me against the Israelites. And when many evils and troubles have befallen them ,this[sacred] song will confront them as a witness ,for it will never be forgotten from the mouths of their descendants.For I know their strong desire and the purpose which they are forming even now ,before I have brought them into the land which I swore to give them .Moses wrote this song the same day and taught It to the Israelites.And Moses spoke in the heearing of all the congregation of Israelites the words of this song until they were ended".(Amplified version).
Tafsiri ya kiswahili ya mistari hii Ni;
"Basi jiandikieni wimbo huu ,uwafundishe wana wa Israeli;ukawatie vinywani mwao ,ili uwe shahidi kwangu wimbo huu ,juu ya wana wa Israeli .Tena itakuwa wakiisha kujiliwa na mambo maovu mengi na mashaka ,utashuhudia wimbo huu mbele Yao kama shahidi ,kwa maana hautasahaulika katika vinywa vya uzao wao;kwani nayajua mawazo Yao wayawazayo hata sasa kabla sijawatia katika nchi niliyowapa.Basi Musa akauandika wimbo huu siku iyo hiyo ,akawafundisha wana wa Israeli.Musa akasema maneno ya wimbo huu masikioni mwa kusanyiko la wana wa Israeli hata yakaisha".
Hiyo Ni mistari katika Biblia Takatifu ,katika mtiririko huu wa kwanza nimetaka tu kukuonesha hii mistari...katika mtiririko utakaofuata nitajaribu kuitolea ufafanuzi hii mistari ili tuone na kutambua wazi kuhusu Biblia Takatifu na Utunzi wa Muziki Mtakatifu(Hususani kwetu sisi watunzi).
Asante.!

Comments

Popular posts from this blog

Biblia inasema nini kuhusu utunzi wa nyimbo takatifu?[#02]

Ndugu katika Kristo,Mwokozi wetu apewe sifa.... Leo tunaendelea na mtiririko wa pili(2) wa somo letu.Katika Mtiririko uliopita tulitoa utangulizi wa Neno kutoka kitabu cha "Kumbukumbu la Torati.31:19-22,30." Leo nitatolea ufafanuzi kuhusu mistrari hii; Jambo la umuhimu la kuona hapa ni kupitia mstari wa 19...Mungu anamwambia Musa "ANDIKA WIMBO HUU" ,katika Biblia ya kiingereza chepesi(Bible in Basic English) ,Neno lililotumika badala ya neno 'andika' ni neno 'tengeneza/kamilisha' ,Kutokana na hayo tuelewe yafuatayo; >Ni jambo la muhimu kwa watunzi/waimbaji kutotengeneza wimbo/nyimbo kwa utaratibu tunaoutaka sisi Bali kwenda kwa gwiji wa Muziki Mtakatifu{ndiye Mungu mwenyewe},ili atupe wimbo/nyimbo yeye mwenyewe[kwa kuwa Musa aliambiwa "ANDIKA" ,Hakujiamulia peke yake]. Fahamu ya kuwa Nyimbo inayotoka kwa Mungu kwenda kwa mtunzi inabeba nguvu(upako) unaoelezewa katika mstari wa 21 kuwa; (a)unakuwa SHAHIDI(ukishuhudia ndani y...

Tumsifu Yesu Kristo.........

Ni tumai langu kuwa nyote mu wazima ,Napenda kukukaribisha katika ukurasa huu, Ni wazo nililokuwa nalo toka kitambo ,kuanzisha ukurasa ambamo kupitia humo nitaweza kuweka mambo muhimu yanihusuyo kama vile nota za tunzi alizoniwezesha Mungu kuzitengeneza ,mashairi n.k ambayo yote kwa ujumla yanaweza kuwa ya msaada kwetu sote ili kulijenga kanisa la Mungu. Huu Ni mwanzo tu ,na taratibu ukurasa huu utakamilika hatua kwa hatua kadiri atakavyowezesha Roho Mtakatifu aliyeianzisha kazi hii. Asante! Anophrine Desdeus Shirima.